April 11, 202510:17:45 AM


RAMADHAN Nswanzurimo, Kocha Mkuu wa Singida United amesema kuwa jana Februari 29 walipaswa waifunge Polisi Tanzania mabao 5-0 ila bahati haikuwa yao kutokana na wachezaji kushindwa kumalizia nafasi walizozipata.

Singida United ilipoteza mchezo wake kwa kufungwa bao 1-0 lililolofungwa na Sixtus Sabilo kwa mkwaju wa penalti huku mkwaju wa Singida United uliopigwa kutokana na mabeki kucheza faulo ndani ya 18 kupanguliwa na Manyika Jr.

Nswanzurimo amesem: "Siwezi kuingia ndani kucheza kwani tulipanga kumaliza mchezo mapema ndani ya kipindi cha kwanza mwisho wa siku ikawa ngumu.

"Tulipata nafasi za kufunga mabao matano na haijawa hivyo sina chaguo kwa kuwa matokeo yameshatokeo,".

Singida United inaendelea kuburuza mkia ikiwa imecheza mechi 25 ina pointi 12 kibindoni.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

Post a Comment

    Author Name

    Contact Form

    Name

    Email *

    Message *

    Powered by Blogger.