April 12, 2025


HARERIMANA Haruna, Kocha Mkuu wa KMC amesema kuwa kwa sasa anahofia kibarua chake kuota nyasi kutokana na mwenendo wa timu yake ulivyo ndani ya Ligi Kuu Bara pamoja na kupigwa chini kwenye Kombe la Shirikisho.

KMC ilitolewa na Kagera Sugar kwenye Kombe la Shirikisho hatua ya 16 bora kwa mikwaju ya penalti 2-0 baada ya dakika 90 kutoshana nguvu.

Kwenye Ligi Kuu Bara KMC ipo nafasi ya 19 ikiwa na pointi 21 baada ya kucheza mechi 24.

"Wachezaji wamekuwa hawanielewi kile ambacho ninawaambia kipindi cha kwanza wanafanya vitu vya kitofauti wanavyovijua wao jambo linalonifanya kipindi cha mapumziko nianze kuwaelekeza upya, nina mashaka huenda mambo yatakuwa magumu ndani ya KMC hasa kwa upande wa nafasi yangu," amesema.

Harerimana alitua KMC akitokea timu ya Lipuli FC ambapo alidai kuwa hakulipwa stahiki zake kwa muda mrefu.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

Post a Comment

    Author Name

    Contact Form

    Name

    Email *

    Message *

    Powered by Blogger.