April 14, 2025

MWINYI Zahera, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa ameona namna wachezaji wake wanavyocheza na kujituma hivyo ana imani msimu ujao watakuwa juu zaidi ya msimu uliopita.

Zahera yupo na timu mkoani Morogoro ikiwa imeweka kambi kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao amesema kuwa ameridhishwa na uwezo wa wachezaji wake wote.

Akizungumza na Saleh Jembe, Zahera amesema kuwa:-"Kuhusu aina ya wachezaji wangu nimewaona kwa ukaribu kuanzia kwenye mechi yao iliyopita na hata mazoezini wote wapo vizuri.

"Wachezaji wangu wana uwezo wa kumiliki mpira na kutoa pasi kwa wakati hivyo msimu ujao tutakuwa juu zaidi ya msimu uliopita," amesema.

Miongoni mwa wachezaji wapya ambao wamesajiliwa msimu huu ndani ya Yanga ni pamoja na Ally Ally, Juma Balinya, Patrick Sibomana, Mapinduzi Balama.

Tags:

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

Post a Comment

    Author Name

    Contact Form

    Name

    Email *

    Message *

    Powered by Blogger.