DANIELE Rugan yupo kwenye hesabu za kusajiliwa na klabu ya Arsenal kwa mkopo akitokea ndani ya kikosi cha Juventus.
Beki huyo msimu uliopita akiwa na Juventus amecheza jumla ya mechi 20 kwenye mashindano yote ya Juventus.
Kwa sasa thamani yake inatajwa kuwa pauni milioni 40 na Meneja wa Arsenal, Unai Emery anaamini atakuwa msaada ndani ya kikosi hicho cha washika bunduki.
Rugani nafasi yake ni finyu kikosi cha kwanza kutokana na Juventus iliyo chini ya Maurizio Sarri kumsajili kinda Matthijs de Ligt kutoka Ajax.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.